WANANCHI WA AMASISHWA KUTUMIA CHUMVI YENYE MADINI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI- HAWA GHASIA amewaagiza Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala na Wakurugenzi wa mikoa ya LINDI na MTWARA kuhakikisha inahamasisha wananchi kutumia chumvi iliyowekwa madini joto ili kupunguza udumavu wa akili kwa watoto. Akitoa agizo hilo mkoani LINDI wakati akifunga mafunzo ya Maafisa Lishe kutoka Nchi nzima Waziri GHASIA amesema utumiaji wa chumvi isiyokuwa na madini joto imeongezeka na kufikia asilimia 92 ambapo kushuka huko kumechangiwa na mikoa ya LINDI na MTWARA. Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wameipongeza serikali na kusema wataenda kuhamasisha jamii umuhimu wa kutumia chumvi yenye madini joto.

Post a Comment

Previous Post Next Post