Siku ya Ijumaa Kuu wakristo nchini waungana na wakristo wengine duniani
kote kuadhimisha siku ya mateso ya Yesu Kristo msalabani.
Katika kuadhimisha sikukuu ya PASAKA Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania JAKAYA KIKWETE ametoa zawadi ya pasaka kwa watoto katika
mahabusu ya watoto ya MWANJELWA iliyopo katikati ya Jiji la MBEYA pamoja
na gereza la watoto la IRAMBO lililopo tarafa ya TEMBELA wilaya ya
MBEYA.
Akikabidhi zawadi hizo kwa niaba ya Rais Mkuu wa wilaya ya MBEYA
NYEREMBE MUNASASABI amesema ni ukarimu wa Rais KIKWETE kutambua jamii
kama hizi ili zijione kuwa ni jamii kama jamii nyingine.
Kwa upande wao walezi wa watoto hao wamemshukuru raisi KIKWETE kwa
kuwakumbuka hasa kipindi hiki cha sikukuu