UDOM YAZINDUA MITAMBO YA KUTAFITI MIAMBA


chuo Kikuu cha Dodoma, UDOM kimezindua Mtambo wa kwanza wa aina yake barani Afrika wa kuchunguza na kutafiti Miamba yenye Madini, Mafuta na Gesi kwa ajili ya kufundishia Wanafunzi wanaosoma Sayansi Ardhi Chuoni hapo. Akizindua Mtambo huo wenye thamani ya Dola milioni moja za Kimarekani, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu hicho, Dr JUMA MWAPACHU amesema kuwa licha ya Kufundishia Chuoni hapo, Mtambo huo utawanufaisha Watanzania na Wachimbaji wa kada zote katika kupima na kuonyesha mahali Miamba ya Madini wanayokusudia kuichima ilipo. Akizungumzia manufaa ya Mtambo huo, Dr MWAPACHU ametaja baadhi ya faida watakazopata Wachimbaji mbali na Wanafunzi ambao watajifunza kwa vitendo namna ya kutafiti Miamba aina mbalimbali kwa ajili ya Madini, Mafuta na Gesi. Ili kuhakikisha kuwa Chuo kinajiongezea mapato kutokana na Mtambo huo, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma Profesa IDRISS KIKULA amesema kuwa Urasimu kwenye utendaji hautapata nafasi

Post a Comment

Previous Post Next Post